7. “Kwa hiyo siku zaja, nasema mimi Mwenyezi-Mungu, ambapo watu hawataapa tena kwa kusema, ‘Kama aishivyo Mwenyezi-Mungu aliyewatoa watu wa Israeli nchini Misri’,
8. bali wataapa kwa kusema, ‘Kama aishivyo Mwenyezi-Mungu aliyewatoa na kuwaongoza Waisraeli kutoka nchi ya kaskazini na kutoka nchi zote ambako aliwatawanya.’ Kisha wataishi katika nchi yao wenyewe.”
9. Kuhusu hao manabii wasiofaa,mimi imevunjika moyo,mifupa yangu yote inatetemeka;nimekuwa kama mlevi,kama mtu aliyelemewa na pombe,kwa sababu yake Mwenyezi-Munguna maneno yake matakatifu.
10. Maana, nchi imejaa wazinzi;kwa sababu ya laana, nchi inaomboleza,na malisho ya nyanda zake yamekauka.Mienendo ya watu ni miovu,nguvu zao zinatumika isivyo halali.
11. Mwenyezi-Mungu asema:“Manabii na makuhani, wote hawamchi Mungu,uovu wao nimeuona hata nyumbani mwangu.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
12. Kwa hiyo njia zao zitakuwa vichochoro vya utelezi gizaniambamo watasukumwa na kuanguka;maana, nitawaletea maafa,ufikapo mwaka wa kuwaadhibu,Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
13. “Miongoni mwa manabii wa Samaria,nimeona jambo la kuchukiza sana:Walitabiri kwa jina la Baaliwakawapotosha watu wangu Waisraeli.
14. Lakini miongoni mwa manabii wa Yerusalemu,nimeona kinyaa cha kutisha zaidi:Wanafanya uzinzi na kusema uongo;wanawaunga mkono wanaotenda maovuhata pasiwe na mtu anayeachana na uovu.Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma;wakazi wake wamekuwa wabaya kama watu wa Gomora.
15. “Kwa hiyo, mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nasema hivi juu ya manabii wa Yerusalemu:Nitawalisha uchungu,na kuwapa maji yenye sumu wanywe.Maana, kutoka kwa manabii wa Yerusalemukutomcha Mungu kumeenea kila mahali nchini.”
16. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi: “Msisikilize maneno ya manabii wanaowatabiria; wanawapeni matumaini ya uongo. Wanayowaambia ni maono yao wenyewe, wala hayakutoka kwangu mimi Mwenyezi-Mungu.
17. Wao hawakomi kuwaambia wale wanaodharau neno langu mimi Mwenyezi-Mungu: ‘Mambo yatawaendea vema.’ Na kumwambia kila mtu afuataye kwa ukaidi fikira zake; ‘Hakuna baya lolote litakalokupata!’”
18. Lakini, ni yupi kati ya manabii haoaliyepata kuhudhuria baraza la Mwenyezi-Mungu,hata akasikia na kuelewa neno lake?Au ni nani aliyejali neno lake,hata akapata kulitangaza?