6. Fahari yote ya watu wa Siyoni imewatoweka;wakuu wake wamekuwa kama kulungu wasio na malisho.Bila nguvu waliwakimbia watesi wao.
7. Ukiwa sasa magofu matupu,Yerusalemu wakumbuka fahari yake.Ulipoangukia mikononi mwa maadui zake,hakuna aliyekuwako kuusaidia.Washindi wake walichekelea kuanguka kwake.
8. Yerusalemu ulitenda dhambi mbaya,ukawa mchafu kwa dhambi zake.Wote waliousifia wanaudharau,maana wameuona uchi wake.Wenyewe wapiga kite na kujificha kwa aibu.
9. Uchafu wake ulionekana waziwazi,lakini wenyewe haukujali mwisho wake.Anguko lake lilikuwa kubwa mno;hakuna awezaye kuufariji.Wasema:“Tazama ee Mwenyezi-Mungu mateso yangu,maana adui yangu ameshinda.”