Kumbukumbu La Sheria 28:17-24 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Vikapu vyenu vya nafaka vitalaaniwa na vyombo vyenu vya kukandia mkate.

18. Watoto wenu watalaaniwa na mazao yenu ya nchi; mifugo yenu italaaniwa isiongezeke.

19. Mtalaaniwa mnapoingia na mnapotoka.

20. “Mwenyezi-Mungu atawaleteeni maafa, vurugu na kukata tamaa katika shughuli zenu zote mpaka mmeangamia upesi kwa sababu ya uovu wa matendo yenu na kwa sababu ya kumwacha Mwenyezi-Mungu.

21. Atawaleteeni maradhi mabaya mpaka wote muangamie kabisa katika nchi ambayo mnaenda kuimiliki.

22. Mwenyezi-Mungu atawashambulia kwa kifua kikuu, homa, majipu, joto kali, ukame, dhoruba na ukungu; mambo hayo yatawaandama mpaka mmeangamia.

23. Mbingu zitakauka kama shaba nyeusi bila mvua, na nchi itakuwa kama chuma.

24. Mwenyezi-Mungu ataifanya vumbi na mchanga kuwa mvua yenu, vumbi litawanyeshea mpaka mmeangamizwa.

Kumbukumbu La Sheria 28