6. Basi, Mwenyezi-Mungu akabadili nia yake,akasema: “Hili pia halitatukia.”
7. Mwenyezi-Mungu alinijalia tena maono mengine: Nilimwona Mwenyezi-Mungu amesimama karibu na ukuta, ameshika mkononi mwake uzi wenye timazi.
8. Naye akaniuliza: “Amosi, unaona nini?” Nikamjibu, “Naona timazi.” Kisha Mwenyezi-Mungu akasema:“Tazama! Naweka timazi kati ya watu wangu Waisraeli.Sitavumilia tena maovu yao.
9. Huko vilimani ambako wazawa wa Isaka hutambikia,kutafanywa kuwa uharibifu mtupuna maskani ya Waisraeli yatakuwa magofu.Nitaushambulia kwa vita ukoo wa mfalme Yeroboamu.”
10. Basi, Amazia kuhani wa mji wa Betheli, akampelekea mfalme Yeroboamu wa Israeli habari hizi: “Amosi analeta fitina juu yako katika ufalme wa Israeli. Hotuba zake ni hatari kwa nchi hii.
11. Anachosema ni hiki:‘Yeroboamu atakufa kwa upanganao Waisraeli watapelekwa uhamishoni,mbali kabisa na nchi yao.’”
12. Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Sasa tumekuchoka, ewe nabii! Nenda zako! Rudi katika nchi ya Yuda, ukatoe unabii huko upate na ujira wako hukohuko.
13. Usitoe tena unabii hapa mjini Betheli, kwa kuwa hapa ni maskani ya ibada ya mfalme; ni hekalu la utawala huu.”
14. Amosi akamjibu Amazia, “Mimi si nabii wa kuajiriwa, wala si mmoja wa kikundi cha manabii. Mimi ni mchungaji na mtunza mikuyu.
15. Mwenyezi-Mungu alinitoa katika kazi yangu hiyo ya uchungaji, akaniamuru nije kuwaambia unabii watu wake wa Israeli.
16. Nawe basi, ewe Amazia,sikiliza neno la Mwenyezi-Mungu:Wewe waniambia nisitoe unabii dhidi ya Israeli,wala nisihubiri dhidi ya wazawa wa Isaka.
17. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:‘Mkeo atakuwa malaya mjini,na wanao wa kiume na kike watauawa vitani.Ardhi yako itagawanywa na kupewa wengine,nawe binafsi utafia katika nchi najisi,nao Waisraeli hakika watapelekwa uhamishoni,mbali kabisa na nchi yao.’”