Yeremia 6:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Enyi watu wa Benyamini,ondokeni Yerusalemu mkimbilie usalama!Pigeni tarumbeta mjini Tekoa;onesheni ishara huko Beth-hakeremu,maana maafa na maangamizi makubwayanakuja kutoka upande wa kaskazini.

2. Mji wa Siyoni ni mzuri na mwororo,lakini utaangamizwa.

3. Watu wataujia kama wachungaji na makundi yao,watapiga hema zao kuuzunguka kila mmoja sehemu yake,wapate kuyaongoza makundi yao.

4. Watasema: “Jitayarisheni kuushambulia Siyoni.Haya! Tuanze kushambulia adhuhuri!Bahati mbaya; jua linatua!Kivuli cha jioni kinarefuka.

5. Basi, tutaushambulia usiku;tutayaharibu majumba yake ya kifalme.”

Yeremia 6