Maombolezo 1:18-20 Biblia Habari Njema (BHN)

18. “Lakini Mwenyezi-Mungu amefanya sawakwa maana nimeliasi neno lake.Nisikilizeni enyi watu wote,yatazameni mateso yangu.Wasichana wangu na wavulana wangu,wamechukuliwa mateka.

19. “Niliwaita wapenzi wangu,lakini wao wakanihadaa.Makuhani na wazee wanguwamefia mjiniwakijitafutia chakula,ili wajirudishie nguvu zao.

20. “Ona, ee Mwenyezi-Mungu nilivyo taabuni.Roho yangu imechafuka,moyo wangu unasononekakwani nimekuasi vibaya.Huko nje kumejaa mauaji,ndani nako ni kama kifo tu.

Maombolezo 1