17. Fahari yake ni fahari ya fahali wa kwanza,pembe zake ni za nyati dume.Atazitumia kuyasukuma mataifa;yote atayasukuma mpaka miisho ya dunia.Efraimu atakuwa na pembe hizo 10,000na Manase kwa maelfu.”
18. Juu ya kabila la Zebuluni na kabila la Isakari, alisema,“Zebuluni, furahi katika safari zako;nawe Isakari, furahi katika mahema yako.
19. Watawaalika wageni kwenye milima yao,na huko watu watatoa sadaka zinazotakiwa.Maana wao watapata utajiri wao kutoka baharinina hazina zao katika mchanga wa pwani.”
20. Juu ya kabila la Gadi, alisema:“Atukuzwe Mungu ampatiaye Gadi sehemu kubwa.Gadi hunyemelea kama simbaakwanyue mkono na utosi wa kichwa.