Kumbukumbu La Sheria 28:3-11 Biblia Habari Njema (BHN)

3. “Miji yenu itabarikiwa na mashamba yenu.

4. “Mtabarikiwa mpate wazawa wengi, mavuno mengi, ng'ombe na kondoo wengi.

5. “Vikapu vyenu vya nafaka vitabarikiwa na vyombo vyenu vya kukandia.

6. Mtabarikiwa mnaporudi nyumbani na mnapotoka nje.

7. Maadui zenu wakiwashambulia, Bwana atawapeni ushindi juu yao. Wakija kuwashambulia kwa njia moja watawakimbieni kwa njia saba.

8. Baraka za Mwenyezi-Mungu zitakuwa katika ghala zenu za nafaka na katika shughuli zenu zote. Atawabariki katika nchi ambayo anawapeni.

9. “Mwenyezi-Mungu atawafanyeni kuwa watu wake watakatifu kama alivyowaahidi, kama mkizitii amri zake yeye Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, na kufuata njia zake.

10. Mataifa yote duniani yakiona kwamba nyinyi mnaitwa kwa jina la Mwenyezi-Mungu yatawaogopa.

11. Mwenyezi-Mungu atawafanikisha kwa wingi: Watoto, mifugo na mavuno shambani katika nchi aliyowaapia wazee wenu kuwa atawapeni,

Kumbukumbu La Sheria 28