Isaya 43:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu aliyewaumba enyi watu wa Yakobo,yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, asema:“Msiogope, maana mimi nimewakomboa;nimewaita kwa jina nanyi ni wangu.

2. Mkipita katika mafuriko,mimi nitakuwa pamoja nanyi;mkipita katika mito,haitawashinda nguvu.Mkitembea katika moto,hamtaunguzwa;mwali wa moto hautawaunguza.

3. Maana mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,Mungu Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu.Nitaitoa nchi ya Misri iwe fidia yenu,nitaitoa Kushi na Seba ili mwachwe huru.

Isaya 43