Isaya 33:18-22 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Mtafikiria tisho lililopita na kujiuliza,“Wako wapi wale waliokadiria na kukisia kodi?Wako wapi wale waliopeleleza ulinzi wetu?”

19. Hamtawaona tena watu wale wenye kiburi,wanaozungumza lugha isiyoeleweka.

20. Tazameni Siyoni tunamofanya sikukuu zetu;tazameni mji Yerusalemu, makao matulivu, hema imara;vigingi vyake havitangolewa kamwe,kamba zake hazitakatwa hata moja.

21. Humo Mwenyezi-Mungu atatuonesha ukuu wake.Kutakuwa na mito mikubwa na vijito,ambamo meli za vita hazitapita,wala meli kubwa kuingia.

22. Maana Mwenyezi-Mungu ni hakimu wetu,yeye ni mtawala wetu;Mwenyezi-Mungu ni mfalme wetu,yeye ndiye anayetuokoa.

Isaya 33