1. Pelekeni wanakondoo kwa mtawala wa nchi,pelekeni kutoka Sela jangwani mpaka mlimani Siyoni.
2. Kama ndege wanavyohangaika na kurukaruka,wakiwa wamefukuzwa kutoka viota vyao,ndivyo walivyo mabinti wa Moabukwenye vivuko vya Arnoni.
3. Wamoabu wanawaambia watu wa Yuda,“Tupeni mwongozo, tuamulieni.Enezeni ulinzi wenu juu yetu,kama vile usiku uenezavyo kivuli chake.Tuficheni sisi wakimbizi;msitusaliti sisi tuliofukuzwa.