Isaya 10:10-14 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Kama nimefaulu kuunyosha mkono wangudhidi ya falme zenye sanamu za miungukubwa kuliko sanamu za Yerusalemu na Samaria;

11. je, nitashindwa kuutenda Yerusalemu na sanamu zake,kama nilivyoutenda Samaria na sanamu zake?”

12. Wakati Mwenyezi-Mungu atakapomaliza kazi zake zote mlimani Siyoni na mjini Yerusalemu, atamwadhibu mfalme wa Ashuru, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.

13. Maana mfalme wa Ashuru alisema:“Kwa nguvu zangu mwenyewe nimetenda hayo,na kwa hekima yangu, maana mimi ni mwerevu!Nimeondoa mipaka kati ya mataifa,nikazipora hazina zao;kama fahali nimewaporomosha walioketia viti vya enzi.

14. Kama mtu anyoshaye mkono kwenye kiota,ndivyo nilivyochukua mali yao;kama mtu aokotavyo mayai yaliyoachwa kiotani,ndivyo nilivyowaokota duniani kote,wala hakuna mtu aliyeweza kupiga bawa,au aliyefungua kinywa kunipigia kelele.”Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:

Isaya 10