Zekaria 6:2-6 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Gari la kwanza lilikokotwa na farasi wekundu, la pili lilikokotwa na farasi weusi,

3. la tatu lilikokotwa na farasi weupe, na la nne lilikokotwa na farasi wa kijivujivu.

4. Basi, nikamwuliza yule malaika aliyeongea nami, “Bwana, magari haya ya farasi yanamaanisha nini?”

5. Malaika akanijibu, “Magari haya ni pepo kutoka pande nne za mbingu. Yalikuwa mbele ya Mwenyezi-Mungu wa dunia nzima, na sasa yanaondoka.

6. Lile gari linalokokotwa na farasi weusi linakwenda kaskazini, lile linalokokotwa na farasi weupe linakwenda magharibi, na lile linalokokotwa na farasi wa kijivujivu linakwenda kusini.”

Zekaria 6