5. bali kila mmoja atasema, ‘Mimi si nabii. Mimi ni mkulima tu; nimeimiliki ardhi tangu ujana wangu’.
6. Na mtu akimwuliza mmoja wao, ‘Vidonda hivi ulivyo navyo mgongoni vimetoka wapi?’ Yeye atajibu, ‘Vidonda hivi nilivipata katika nyumba ya rafiki zangu.’”
7. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:“Amka, ee upanga!Inuka umshambulie mchungaji wangu;naam, mchungaji anayenitumikia.Mpige mchungaji na kondoo watawanyike.Nitaunyosha mkono wangu,kuwashambulia watu wadhaifu.
8. Theluthi mbili za watu katika nchi zitaangamizwa;ni theluthi moja tu itakayosalimika.
9. Theluthi hiyo moja itakayosalia,nitaijaribu na kuitakasa,kama mtu asafishavyo fedha,naam, kama ijaribiwavyo dhahabu.Hapo wao wataniomba mimi,nami nitawajibu.Nitasema, ‘Hawa ni watu wangu’,nao watasema, ‘Mwenyezi-Mungu, ndiye Mungu wetu.’”