1. Laiti kichwa changu kingekuwa kisima cha maji,na macho yangekuwa chemchemi ya machoziili nipate kulia mchana na usiku,kwa ajili ya watu wangu waliouawa!
2. Laiti ningekuwa na mahali pa kukaa jangwani,ambamo ningewaacha watu wangu na kwenda zangu.”Mwenyezi-Mungu asema:“Wote ni watu wazinzi,ni genge la watu wahaini.
3. Hupinda maneno yao kama pinde;wameimarika kwa uongo na si kwa haki.Huendelea kutoka uovu hata uovu,wala hawanitambui mimi.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
4. Kila mmoja ajihadhari na jirani yake!Hata ndugu yeyote haaminiki,kila ndugu ni mdanganyifu,na kila jirani ni msengenyaji.
5. Kila mmoja humdanganya jirani yake,hakuna hata mmoja asemaye ukweli.Wamezifundisha ndimi zao kusema uongo;hutenda uovu kiasi cha kushindwa kabisa kutubu.