17. Watayala mazao yenu na chakula chenu;watawamaliza watoto wenu wa kike na wa kiume.Watachinja makundi yenu ya kondoo na ng'ombe;wataiharibu mizabibu yenu na mitini yenu.Miji yenu ya ngome mnayoitegemea,wataiharibu kwa silaha zao.
18. “Lakini, hata katika siku hizo mimi Mwenyezi-Mungu nasema, sitawaangamiza na kuwamaliza kabisa.
19. Na watu wenu watakapouliza ‘Kwa nini Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ametutendea mambo hayo yote?’ Wewe utawaambia, ‘Nyinyi mlimwacha Mwenyezi-Mungu, mkaitumikia miungu ya kigeni katika nchi yenu. Basi ndivyo mtakavyowatumikia watu wengine katika nchi isiyo yenu.’