Yeremia 48:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi:“Ole watu wa Nebo, maana mji wake umeharibiwa!Kiriathaimu umeaibishwa, umetekwa,ngome yake imebomolewa mbali;

2. fahari ya Moabu imetoweka.Mpango ulifanywa huko Heshboni dhidi yake:‘Haya! Tuwaangamize wasiwe tena taifa!’Nawe Madmeni utanyamazishwa,upanga utakufuatia.

3. Sikiliza! Kilio kutoka Horonaimu:‘Maangamizi na uharibifu mkubwa!’

4. Moabu tayari imeangamizwakilio chake chasikika mpaka Soari.

5. Walionusurika wanapanda kwenda Luhithihuku wanalia kwa sauti.Wanapoteremka kwenda Horonaimu,wanasikia kilio cha uharibifu.

Yeremia 48