Wimbo Ulio Bora 1:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Msinishangae kwa sababu ni mweusi,maana jua limenichoma.Ndugu zangu walinikasirikia,wakanifanya mlinzi wa mashamba ya mizabibu.Lakini sikutunza shamba langu la mizabibu.

7. Hebu niambie ee wangu wa moyo,utawalisha wapi kondoo wako?Ni wapi watakapopumzikia adhuhuri?Kwa nini mimi nikutafutekati ya makundi ya wenzako?

8. Ewe upendezaye kuliko wanawake wote;kama hujui, fanya hivi:Zifuate nyayo za kondoo;basi, walishe mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.

9. Wewe ee mpenzi wangu,nakulinganisha na farasi dume wa magari ya Farao.

10. Mashavu yako yavutia kwa vipuli,na shingo yako kwa mikufu ya johari.

11. Lakini tutakufanyizia mikufu ya dhahabu,iliyopambwa barabara kwa fedha.

Wimbo Ulio Bora 1