Waebrania 8:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa Israeli siku zijazo, asema Bwana:Nitaweka sheria zangu akilini mwao,na kuziandika mioyoni mwao.Mimi nitakuwa Mungu wao,nao watakuwa watu wangu.

11. Hakuna atakayemfundisha mwananchi mwenzake,wala atakayemwambia ndugu yake:‘Mjue Bwana’.Maana wote, wadogo na wakubwa, watanijua mimi.

12. Nitawasamehe makosa yao,wala sitakumbuka tena dhambi zao.”

13. Kwa kusema juu ya agano jipya, Mungu alilichakaza lile la kwanza; na chochote kinachochakaa na kuwa kikuukuu kitatoweka karibuni.

Waebrania 8