8. Ukamwona kuwa yu mwadilifu mbele yako;ukafanya agano naye kuwapa wazawa wake nchi ya Wakanaani,Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgashi.Na ahadi yako ukaitimiza;kwani wewe u mwaminifu.
9. “Uliyaona mateso ya babu zetuwalipokuwa nchini Misri,na walipokuomba msaada kwenye Bahari ya Shamuuliwasikia.
10. Ulifanya ishara na maajabu dhidi ya Farao,watumishi wake wotena watu wote wa nchi yake;kwani ulijua kuwawaliwakandamiza babu zetu.Ukajipatia umaarufu uliopo mpaka leo.
11. Uliigawa bahari katikati mbele yao,nao wakapita katikati ya bahari,mahali pakavu.Lakini ukawatupa Wamisri waliowafuatiakama jiwe zito ndani ya maji mengi.
12. Mchana uliwaongoza kwa mnara wa wingu,na usiku uliwaongoza kwa mnara wa motoili kuwamulikia njia ya kuendea.
13. Kule mlimani Sinaiulishuka toka mbinguni na kuzungumza nao.Ukawapa maagizo safi, sheria za kweli,kanuni nzuri na amri.
14. Kwa njia ya Mose, mtumishi wako,ukawajulisha Sabato yako takatifuna ukawaagiza kuzifuata amri,kanuni na sheria ulizowaamrisha.
15. Walipokuwa na njaa,ukawapa chakula kutoka mbinguni.Walipokuwa na kiuukawapa maji kutoka kwenye mwamba.Ukawaagiza kuichukua nchi uliyokuwa umewaahidi.
16. Lakini wao na babu zetu wakawa na kiburina wakawa na shingo ngumuwakakataa kufuata maagizo yako.
17. Wakakataa kutii;wasiyakumbuke maajabu uliyofanya miongoni mwao.Wakawa na shingo zao ngumu,wakajichagulia kiongozi wa kuwarudishautumwani nchini Misri.Bali wewe Mungu u mwepesi kusamehe,mwenye neema na huruma,wewe hukasiriki upesi.U mwenye fadhili nyingi, na hukuwatupa.
18. Hata walipojitengenezea sanamu ya ndama na kusema,‘Huyu ndiye mungu wetualiyetutoa kutoka nchi ya Misri,’wakawa wamefanya kufuru kubwa.