Mwanzo 48:10-16 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee. Basi, Yosefu akawasogeza wanawe karibu na baba yake, naye akawabusu na kuwakumbatia.

11. Kisha Israeli akamwambia Yosefu, “Sikutazamia kuuona uso wako tena; lakini, kumbe, Mungu amenijalia hata kuwaona watoto wako!”

12. Hapo Yosefu akawaondoa wanawe kwenye magoti ya baba yake, kisha akainama kwa heshima.

13. Yosefu akawainua wanawe wawili, Efraimu katika mkono wake wa kulia, akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa baba yake, na Manase katika mkono wake wa kushoto, akimwelekeza kwenye mkono wa kulia wa baba yake, akawasogeza kwa babu yao.

14. Lakini Israeli akaipishanisha mikono yake: Mkono wake wa kulia akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza.

15. Kisha Israeli akambariki Yosefu, akisema,“Mungu ambaye babu zanguAbrahamu na Isaka walimtii maishani mwao,Mungu ambaye ameniongoza maishani mwangu hadi leo,

16. na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote,na awabariki vijana hawa!Jina langu na majina ya wazee wangu, Abrahamu na Isaka,yadumishwe katika vijana hawa;nao waongezeke kwa wingi duniani.”

Mwanzo 48