Mathayo 11:26-30 Biblia Habari Njema (BHN)

26. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.

27. “Baba yangu amenikabidhi vitu vyote. Hakuna amjuaye Mwana ila Baba, wala amjuaye Baba ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anapenda kumfunulia.

28. Njoni kwangu nyinyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29. Jifungeni nira yangu, mkajifunze kwangu, maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo, nanyi mtatulizwa rohoni mwenu.

30. Maana, nira niwapayo mimi ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.”

Mathayo 11