6. Hekalu lake amelibomoa kama kitalu bustanini,maskani yake ameiharibu.Amefutilia mbali sikukuu na Sabato huko Siyoni,kwa hasira yake kuu amewakataa mfalme na makuhani.
7. Mwenyezi-Mungu ameipuuza madhabahu yakena hekalu lake amelikataa.Kuta za majumba mjini amewaachia maadui wazibomoe,wakapiga kelele humo nyumbani kwa Mwenyezi-Mungukama kelele za wakati wa sikukuu.
8. Mwenyezi-Mungu alipania kuubomoa ukuta wa mji wa Siyoni;aliupima na kuhakikisha kila kitu kimeharibiwa;minara na kuta za nje ya mji akazifanya ukiwa,zote kwa pamoja zikaangamia.
9. Malango yake yameanguka chini,makomeo yake ameyaharibu na kuyavunjavunja.Mfalme na wakuu wake wako uhamishoni kati ya mataifa.Mwongozo wa sheria umetoweka kabisa,manabii wake hawapati tena maonokutoka kwake Mwenyezi-Mungu.
10. Wazee wa Siyoni wameketi chini kimya,wamejitia mavumbi vichwanina kuvaa mavazi ya gunia.Wasichana wa Yerusalemu wameinamisha vichwa.
11. Macho yangu yamevimba kwa kulia,roho yangu imechafuka.Moyo wangu una huzuni nyingikwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangukwa sababu watoto wachanga wanazirai katika barabara za mji.