Kumbukumbu La Sheria 8:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Wakati huo wa miaka arubaini nguo zenu hazikuchakaa, wala miguu yenu haikuvimba.

5. Kumbukeni kwamba Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, anawarudi kama vile baba amrudivyo mwanawe.

6. Hivyo, shikeni amri za Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, mpate kuzifuata njia zake na kumcha yeye.

7. Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu anawaleteni kwenye nchi nzuri, nchi yenye vijito na chemchemi, na maji yabubujikayo kutoka bondeni na milimani;

8. nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu, mitini, mikomamanga, mizeituni na asali.

Kumbukumbu La Sheria 8