1. Hii ndiyo baraka ambayo Mose, mtu wa Mungu aliwatakia Waisraeli kabla ya kufariki kwake. Alisema:
2. Mwenyezi-Mungu alikuja kutoka mlima Sinai,alitutokea kutoka mlima Seiri;aliiangaza kutoka mlima Parani.Alitokea kati ya maelfu ya malaika,na moto uwakao katika mkono wake wa kulia.
3. Mwenyezi-Mungu aliwapenda watu wake;na huwalinda watakatifu wake wote.Hivyo, malaika wake walifuata nyayo zake,na kupata maagizo kutoka kwake.
4. Mose alituamuru tutii sheria;kitu cha thamani kuu cha taifa letu.
5. Mwenyezi-Mungu akawa mfalme wa Israeli,wakati viongozi wao walipokutana,na makabila yote yalipokusanyika.
6. Mose alisema juu ya kabila la Reubeni:“Reubeni aishi wala asife,na watu wake wasiwe wachache.”
7. Juu ya kabila la Yuda alisema:“Ee Mwenyezi-Mungu usikilize kilio cha kabila la Yuda;umrudishe tena kwa watu wale wengine.Upigane kwa mikono yako kwa ajili yake,ulisaidie kabila la Yuda dhidi ya adui zake.”
8. Juu ya kabila la Lawi, alisema:“Ee Mwenyezi-Mungu ulipatie Lawi kauli yako ya Urimu,kauli yako ya thumimu kwa hao waaminifu wako,ambao uliwajaribu huko Masa.