Kumbukumbu La Sheria 32:38-41 Biblia Habari Njema (BHN)

38. Iko wapi hiyo miungu iliyokula matoleo yenuna kunywa divai na tambiko zenu za kinywaji?Basi na iinuke, iwasaidieni;acheni hiyo iwe kinga yenu sasa!

39. Oneni kuwa mimi ndimi Munguna wala hakuna mwingine ila mimi.Mimi huua na kuweka hai;hujeruhi na kuponya,na hakuna awezaye kumwokoa yeyote mikononi mwangu.

40. Nanyosha mkono wangu mbinguni,na kuapa, kwa uhai wangu wa milele,

41. kama mkiuona upanga wangu umeremetao,na kunyosha mkono kutoa hukumu,nitawalipiza kisasi maadui zangu,nitawaadhibu wale wanaonichukia.

Kumbukumbu La Sheria 32