14. bila kugeuka kulia au kushoto kuifuata miungu mingine na kuitumikia.
15. “Lakini kama hamtaitii sauti ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, au msipokuwa waangalifu kutekeleza amri zake zote na masharti ninayowaamuru leo, basi mtapatwa na laana hizi zote:
16. Mtapata laana katika miji yenu na mashamba yenu.
17. Vikapu vyenu vya nafaka vitalaaniwa na vyombo vyenu vya kukandia mkate.
18. Watoto wenu watalaaniwa na mazao yenu ya nchi; mifugo yenu italaaniwa isiongezeke.
19. Mtalaaniwa mnapoingia na mnapotoka.
20. “Mwenyezi-Mungu atawaleteeni maafa, vurugu na kukata tamaa katika shughuli zenu zote mpaka mmeangamia upesi kwa sababu ya uovu wa matendo yenu na kwa sababu ya kumwacha Mwenyezi-Mungu.
21. Atawaleteeni maradhi mabaya mpaka wote muangamie kabisa katika nchi ambayo mnaenda kuimiliki.