7. “Mtu yeyote akimwiba Mwisraeli mwenzake na kumfanya mtumwa wake au kumwuza utumwani, mtu huyo lazima auawe. Ndivyo mtakavyokomesha uovu miongoni mwenu.
8. “Kama mtu akishikwa na ukoma mnapaswa kuwa waangalifu kufuata maagizo ya Walawi. Kama nilivyowaamuru ndivyo mtakavyofuata kwa uangalifu.
9. Kumbukeni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu alivyomtendea Miriamu mlipokuwa safarini kutoka Misri.
10. “Ukimkopesha jirani kitu chochote, usiingie kwake kuchukua rehani.
11. Msubiri nje na umwache yeye mwenyewe akuletee hiyo rehani.
12. Kama yeye ni maskini usikae na rehani hiyo usiku kucha.