Kumbukumbu La Sheria 22:9-14 Biblia Habari Njema (BHN)

9. “Usipande mizabibu yako pamoja na mimea mingine, la sivyo mazao yote yatakuwa haramu, siyo tu yale uliyopanda bali pia matunda ya mizabibu.

10. “Usilime shamba kwa kutumia ng'ombe na punda pamoja.

11. “Usivae mavazi yaliyofumwa kwa sufu na kitani.

12. “Funga vishada katika pembe nne za vazi lako.

13. “Mwanamume akioa mwanamke, halafu baadaye akate shauri kumwacha,

14. na kumshtaki kwamba ametenda mambo ya aibu, na kumharibia sifa kwa kusema kwamba hakupata ushahidi wa ubikira wakati alipomwoa,

Kumbukumbu La Sheria 22