2. Panua nafasi hemani mwako,tandaza mapazia hapo unapoishi,usijali gharama zake.Zirefushe kamba zake,na kuimarisha vigingi vyake;
3. maana utapanuka kila upande;wazawa wako watamiliki mataifa,miji iliyokuwa mahame itajaa watu.
4. Usiogope maana hutaaibishwa tena;usifadhaike maana hutadharauliwa tena.Utaisahau aibu ya ujana wako,wala hutaikumbuka tena fedheha ya ujane wako.
5. Muumba wako atakuwa mume wako;Mwenyezi-Mungu wa majeshi, ndilo jina lake,Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako;yeye aitwa ‘Mungu wa ulimwengu wote’.