Isaya 35:3-6 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Imarisheni mikono yenu dhaifu,kazeni magoti yenu manyonge.

4. Waambieni waliokufa moyo:“Jipeni moyo, msiogope!Tazameni Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi,atakuja kuwaadhibu maadui zenu;atakuja yeye mwenyewe kuwaokoeni.”

5. Hapo vipofu wataona tena,na viziwi watasikia tena.

6. Walemavu watarukaruka kama paa,na bubu wataimba kwa furaha.Maji yatabubujika nyikanina vijito vya maji jangwani.

Isaya 35