1. Ole wako ewe mwangamizi,unayeangamiza bila wewe kuangamizwa!Ole wako wewe mtenda hila,ambaye hakuna aliyekutendea hila!Utakapokwisha kuangamizawewe utaangamizwa!Utakapomaliza kuwatendea watu hilawewe utatendewa hila.
2. Ee Mwenyezi-Mungu, utuonee huruma,kwako tumeliweka tumaini letu.Uwe kinga yetu kila siku,wokovu wetu wakati wa taabu.
3. Kwa kishindo cha sauti yako watu hukimbia;unapoinuka tu, mataifa hutawanyika.
4. Maadui zao wanakusanya mateka,wanayarukia kama panzi.
5. Mwenyezi-Mungu ametukuka,yeye anaishi juu mbinguni.Ameujaza Siyoni haki na uadilifu.
6. Enyi watu wa Yerusalemu,Mwenyezi-Mungu atawajalieni usalama,atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa.Hazina yenu kuu ni kumcha Mwenyezi-Mungu.
7. Haya, mashujaa wao wanalia,wajumbe wa amani wanaomboleza.
8. Barabara kuu zimebaki tupu;hamna anayesafiri kupitia humo.Mikataba inavunjwa ovyo,mashahidi wanadharauliwa.Hamna anayejali tena maisha ya binadamu.
9. Nchi inaomboleza na kunyauka;misitu ya Lebanoni imekauka,bonde zuri la Sharoni limekuwa jangwa,huko Bashani na mlimani Karmelimiti imepukutika majani yake.
10. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Sasa mimi nitainuka;sasa nitajiweka tayari;sasa mimi nitatukuzwa.
11. Mipango yenu yote ni kama makapi,na matokeo yake ni takataka tupu.Pumzi yangu itawaangamiza kama moto.