18. Atakayeikimbia hofu atatumbukia shimoni;atakayetoka shimoni atanaswa mtegoni.Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa,misingi ya dunia inatikisika.
19. Dunia inavunjikavunjika,inapasuka na kutikiswatikiswa.
20. Inapepesuka kama mlevi,inayumbayumba kama kibanda.Imelemewa na mzigo wa dhambi zakenayo itaanguka wala haitainuka tena.
21. Siku ile Mwenyezi-Mungu ataliadhibu jeshi la anganikadhalika na wafalme wa duniani.