Isaya 22:10-13 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Mlizikagua nyumba za mji wa Yerusalemu, mkabomoa baadhi yake ili kupata mawe ya kuimarisha kuta za mji.

11. Katikati ya kuta hizo mlijijengea birika la kuhifadhia maji yanapotiririka kutoka bwawa la zamani. Lakini hamkumtafuta Mungu aliyepanga mambo haya yote; hamkumjali yeye aliyepanga hayo yote tangu zamani.

12. Siku hiyo, Mwenyezi-Mungu, wa majeshialiwataka mlie na kuomboleza,mnyoe nywele na kuvaa mavazi ya gunia.

13. Lakini nyinyi mkafurahi na kusherehekea.Mlichinja ng'ombe na kondoo,mkala nyama na kunywa divai.Nyinyi mlisema:“Acha tule na kunywamaana kesho tutakufa.”

Isaya 22