5. Toeni tambiko ya shukrani ya mikate iliyochachushwa.Tangazeni popote kwamba mmetoa kwa hiari;kwani ndivyo mnavyopenda kufanya!Mimi Bwana Mungu nimenena.
6. “Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna,nikasababisha ukosefu wa chakula popote.Hata hivyo hamkunirudia.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
7. “Tena niliwanyima mvuamiezi mitatu tu kabla ya mavuno.Niliunyeshea mvua mji mmoja,na mji mwingine nikaunyima.Shamba moja lilipata mvua,na lingine halikupata, likakauka.
8. Watu wa miji miwili, mitatu wakakimbilia mji mwingine,wapate maji, lakini hayakuwatosha.Hata hivyo hamkunirudia.Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.