2 Samueli 10:15-17 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Lakini Waaramu walipoona kwamba wameshindwa na Waisraeli, walijikusanya pamoja.

16. Hadadezeri aliagiza Waaramu waliokuwa ngambo ya mto Eufrate waletwe, wapelekwe huko Helamu wakiongozwa na Shobaki kamanda wa jeshi la Hadadezeri.

17. Daudi alipopata habari, aliwakusanya pamoja Waisraeli wote, akavuka mto Yordani na kwenda mpaka Helamu. Nao Waaramu walijipanga tayari kwa vita dhidi ya Daudi, wakaanza kupigana naye.

2 Samueli 10