1. Ndugu, kuhusu vipaji vya kiroho, napenda mfahamu vizuri mambo haya:
2. Mnajua kwamba, kabla ya kuongoka kwenu, mlitawaliwa na kupotoshwa na sanamu tupu.
3. Basi, jueni kwamba mtu yeyote anayeongozwa na Roho wa Mungu hawezi kusema: “Yesu alaaniwe!” Hali kadhalika, mtu yeyote hawezi kusema: “Yesu ni Bwana,” asipoongozwa na Roho Mtakatifu.
4. Vipaji vya kiroho ni vya namna nyingi, lakini Roho avitoaye ni mmoja.