Wim. 8:5-10 Swahili Union Version (SUV)

5. Ni nani huyu apandaye kutoka nyikani,Akimtegemea mpendwa wake?Nalikuamsha chini ya huo mpera;Huko mama yako alikuonea utungu,Aliona utungu aliyekuzaa.

6. Nitie kama muhuri moyoni mwako,Kama muhuri juu ya mkono wako;Kwa maana upendo una nguvu kama mauti,Na wivu ni mkali kama ahera.Mwako wake ni mwako wa moto,Na miali yake ni miali ya Yahu.

7. Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo,Wala mito haiwezi kuuzamisha;Kama mtu angetoa badala ya upendoMali yote ya nyumbani mwake,Angedharauliwa kabisa.

8. Kwetu sisi tuna umbu mdogo,Wala hana maziwa;Tumfanyieje umbu letu,Siku atakapoposwa?

9. Kama akiwa tu ukuta,Tumjengee buruji za fedha;Na kama akiwa ni mlango,Tumhifadhi kwa mbao za mierezi.

10. Mimi nalikuwa ukuta,Na maziwa yangu kama minara;Ndipo nikawa machoni pakeKama mtu aliyeipata amani.

Wim. 8