Wim. 7:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Siti msharifu, jinsi zilivyo nzuriHatua zako katika mitalawanda.Mapaja yako ya mviringo ni kama johari,Kazi ya mikono ya fundi mstadi;

2. Kitovu chako ni kama bilauri iliyoviringana,Na isikose divai iliyochanganyika;Tumbo lako ni mfano wa chungu ya ngano,Iliyozungukwa na ugo wa nyinyoro;

3. Maziwa yako mawili ni kama wana-paa wawili,Ambao ni mapacha ya paa;

4. Shingo yako ni kama huo mnara wa pembe;Macho yako kama viziwa vya Heshboni,Karibu na mlango wa Beth-rabi;Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni,Unaoelekea Dameski;

5. Kichwa chako juu yako ni kama Karmeli,Na nywele za kichwa chako kama urujuani,Mfalme amenaswa na mashungu yake.

Wim. 7