7. Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka;Ameufanya mnyororo wangu mzito.
8. Naam, nikilia na kuomba msaada,Huyapinga maombi yangu.
9. Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa;Ameyapotosha mapito yangu.
10. Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye,Kama simba aliye mafichoni.
11. Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua;Amenifanya ukiwa.
12. Ameupinda upinde wake,Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.
13. Amenichoma viunoKwa mishale ya podo lake.
14. Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote;Wimbo wao mchana kutwa.
15. Amenijaza uchungu,Amenikinaisha kwa pakanga.
16. Amenivunja meno kwa changarawe;Amenifunika majivu.
17. Umeniweka nafsi yangu mbali na amani;Nikasahau kufanikiwa.
18. Nikasema, Nguvu zangu zimepotea,Na tumaini langu kwa BWANA.
19. Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu,Pakanga na nyongo.
20. Nafsi yangu ikali ikiyakumbuka hayo,Nayo imeinama ndani yangu.
21. Najikumbusha neno hili,Kwa hiyo nina matumaini.