Omb. 3:42-61 Swahili Union Version (SUV)

42. Sisi tumekosa na kuasi;Wewe hukusamehe.

43. Umetufunika kwa hasira na kutufuatia;Umeua, wala hukuona huruma.

44. Umejifunika nafsi yako kwa wingu,Maombi yetu yasipite.

45. Umetufanya kuwa takataka, na vifusiKatikati ya mataifa.

46. Juu yetu adui zetu woteWametupanulia vinywa vyao.

47. Hofu imetujilia na shimo,Ukiwa na uharibifu.

48. Jicho langu lachuruzika mito ya majiKwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu.

49. Jicho langu latoka machozi lisikome,Wala haliachi;

50. Hata BWANA atakapoangaliaNa kutazama toka mbinguni.

51. Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu,Kwa sababu ya binti zote za mji wangu.

52. Walio adui zangu bila sababuWameniwinda sana kama ndege;

53. Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani,Na kutupa jiwe juu yangu.

54. Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu,Nikasema, Nimekatiliwa mbali.

55. Naliliitia jina lako, BWANA, kutoka lile shimoLiendalo chini kabisa.

56. Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lakoIli usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu.

57. Ulinikaribia siku ile nilipokulilia;Ukasema, Usiogope.

58. Ee BWANA umenitetea mateto ya nafsi yangu;Umeukomboa uhai wangu.

59. Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee BWANA;Unihukumie neno langu.

60. Umekiona kisasi chao chote,Na mashauri yao yote juu yangu.

61. Ee BWANA, umeyasikia matukano yao,Na mashauri yao yote juu yangu;

Omb. 3