41. Na tumwinulie Mungu aliye mbinguniMioyo yetu na mikono.
42. Sisi tumekosa na kuasi;Wewe hukusamehe.
43. Umetufunika kwa hasira na kutufuatia;Umeua, wala hukuona huruma.
44. Umejifunika nafsi yako kwa wingu,Maombi yetu yasipite.
45. Umetufanya kuwa takataka, na vifusiKatikati ya mataifa.
46. Juu yetu adui zetu woteWametupanulia vinywa vyao.