Omb. 3:3-8 Swahili Union Version (SUV)

3. Hakika juu yangu augeuza mkono wakeMara kwa mara mchana wote.

4. Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu;Ameivunja mifupa yangu.

5. Amejenga boma juu yangu,Na kunizungusha uchungu na uchovu.

6. Amenikalisha penye giza,Kama watu waliokufa zamani.

7. Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka;Ameufanya mnyororo wangu mzito.

8. Naam, nikilia na kuomba msaada,Huyapinga maombi yangu.

Omb. 3