2. Ameniongoza na kuniendesha katika gizaWala si katika nuru.
3. Hakika juu yangu augeuza mkono wakeMara kwa mara mchana wote.
4. Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu;Ameivunja mifupa yangu.
5. Amejenga boma juu yangu,Na kunizungusha uchungu na uchovu.
6. Amenikalisha penye giza,Kama watu waliokufa zamani.
7. Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka;Ameufanya mnyororo wangu mzito.