17. Amka, amka, simama, Ee Yerusalemu,Wewe uliyenywea, mkononi mwa BWANA,Kikombe cha hasira yake;Bakuli la kikombe cha kulevya-levyaUmelinywea na kulimaliza.
18. Hapana hata mmoja wa kumwongozaMiongoni mwa wana wote aliowazaa,Wala hapana hata mmoja wa kumshika mkonoMiongoni mwa wana wote aliowalea.
19. Mambo haya mawili yamekupata;Ni nani awezaye kukusikitikia?Ukiwa na uharibifu, na njaa na upanga;Niwezeje kukutuliza?