Ayu. 30:12-20 Swahili Union Version (SUV)

12. Kwa mkono wangu wa kuume huinuka kundi;Huisukuma miguu yangu kando,Na kunipandishia njia zao za uharibifu.

13. Waiharibu njia yangu,Wauzidisha msiba wangu,Watu wasio na msaidizi.

14. Wanijilia kama wapitao katika ufa mpana;Katikati ya magofu wanishambulia.

15. Vitisho vimenigeukia;Huifukuza heshima yangu kama upepo;Na kufanikiwa kwangu kumepita kama wingu.

16. Sasa nafsi yangu inamwagika ndani yangu;Siku za mateso zimenishika.

17. Wakati wa usiku mifupa yangu huchomeka ndani yangu,Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki.

18. Kwa ugonjwa wangu kuwa na nguvu nyingiMavazi yangu yameharibika;Hunikaza kama shingo ya kanzu yangu.

19. Yeye amenibwaga topeni,Nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.

20. Nakulilia wewe, wala huniitikii;Nasimama, nawe wanitazama tu.

Ayu. 30