Ayu. 30:11-17 Swahili Union Version (SUV)

11. Kwani ameilegeza kamba yake, na kunitesa,Wala hawajizuii tena mbele yangu.

12. Kwa mkono wangu wa kuume huinuka kundi;Huisukuma miguu yangu kando,Na kunipandishia njia zao za uharibifu.

13. Waiharibu njia yangu,Wauzidisha msiba wangu,Watu wasio na msaidizi.

14. Wanijilia kama wapitao katika ufa mpana;Katikati ya magofu wanishambulia.

15. Vitisho vimenigeukia;Huifukuza heshima yangu kama upepo;Na kufanikiwa kwangu kumepita kama wingu.

16. Sasa nafsi yangu inamwagika ndani yangu;Siku za mateso zimenishika.

17. Wakati wa usiku mifupa yangu huchomeka ndani yangu,Na maumivu yanayonitafuna hayapumziki.

Ayu. 30