Ayu. 30:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Lakini sasa hao walio wadogo wangu hunifanyia mzaha,Ambao baba zao niliwadharau hata kuwaweka na mbwa wa kundi langu.

2. Naam, uwezo wa mikono yao utanifaa nini?Watu ambao nguvu zao zimekoma.

3. Wamekonda kwa uhitaji na njaa;Huguguna nchi kavu, penye giza la ukiwa na uharibifu.

4. Hung’oa mboga ya chumvi kwenye kichaka;Na mizizi ya mretemu ni chakula chao.

5. Hufukuzwa watoke kati ya watu;Huwapigia kelele kama kumpigia mwivi.

6. Lazima hukaa katika mianya ya mabonde,Katika mashimo ya nchi na ya majabali.

7. Hulia kama punda vichakani;Hukusanyika chini ya upupu.

Ayu. 30