1. Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka ishirini na kenda; na jina la mamaye aliitwa Abiya binti Zekaria.
2. Akafanya yaliyo ya adili machoni pa BWANA, sawasawa na yote aliyoyafanya Daudi babaye.