2 Nya. 28:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Ahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na sita; wala hakufanya yaliyo ya adili machoni pa BWANA, kama Daudi babaye;

2. bali akaziendea njia za wafalme wa Israeli, akawafanyizia mabaali sanamu za kusubu.

3. Tena akafukiza uvumba katika bonde la mwana wa Hinomu, akawateketeza wanawe motoni, sawasawa na machukizo ya mataifa, aliowafukuza BWANA mbele ya wana wa Israeli.

2 Nya. 28